Lugha Isiyosemwa

Jaribio la Upole wa Kibinadamu

Lugha Isiyosemwa — a story by Pemba Umoja

Mvulana mdogo alisimama kwenye ukingo wa gati kando ya mto mrefu, wenye kupinda. Meli mbili zilikuwa zinakuja upande wake. Mvulana alikuwa tayari kuanza jaribio lake la upole wa kibinadamu.

Meli ya kwanza ilipokaribia, alitabasamu kwa upana kadri alivyoweza na kupunga mkono wake kusema habari. Hakuna mtu hata mmoja kwenye meli ya kwanza aliyemrudishia salamu. Kila abiria alimtazama mwenzake kwa jicho la pembeni. Katika lugha isiyosemwa, waliamua kutofanya chochote, kumtazama mvulana mdogo akipunga mkono kutoka gatini na kutofanya chochote, kuendelea na mazungumzo yao kana kwamba mvulana kwenye ukingo wa gati hakuonekana.

Kisha meli ya pili ikaja. Tena, mvulana alitabasamu kutoka sikio hadi sikio na kuinua mkono wake juu kupunga. Watu wengi walimrudishia salamu. Walipunga mikono wakiwa na tabasamu pana zikichomoza kwenye midomo yao. Roho tofauti ilikuwa inawapitia mishipani. Walizungumza lugha isiyosemwa tofauti.

A story by Pemba Umoja