Jaribu

Mvulana, Hekalu, na Jina Alilopewa

Jaribu — a story by Pemba Umoja

Jaribu alifungua mlango wa hekalu.

Alimwona tumbili wa dhahabu mwenye macho ya rangi ya machungwa.

Tumbili alizungumza naye.

“Jina lako nani?” aliuliza.

“Jaribu,” mvulana akanong’ona.

“Usinitanie,” akasema tumbili.

“La. ‘Jaribu’ ndilo jina langu. Wazazi wangu walinipa ili nikumbushwe daima na kila mtu anayeniita kwa jina langu kujaribu, nisikate tamaa.”

“Una wazazi wenye hekima sana,” akasema tumbili, macho yake yakibadilika kutoka rangi ya machungwa hadi nyekundu. “Naweza kuwaona sasa.”

“Wako wapi?” akauliza Jaribu. “Wameshafariki,” akasema kwa huzuni, chozi likimtoka kwenye pembe ya jicho.

“Nawaona mahali penye utulivu,” akajibu tumbili. “Wanatabasamu.”

“Nawakumbuka,” akanong’ona Jaribu.

“Wazazi wako wanakuchunga daima,” akajibu tumbili, “na wanajivunia sana kwamba umeliheshimu jina walilokupa.”

A story by Pemba Umoja