Wazimu wa Usiku wa Manane

Mwezi Mpevu Juu ya Mkahawa wa Kileleni

Wazimu wa Usiku wa Manane — a story by Pemba Umoja

Mkahawa wa Mwezi Mpevu ulikuwa kilele cha mlima. Vilele vyenye ncha kali viliinuka juu ya pwani kama miiba ya fenesi. Mbalamwezi ilimetameta juu ya bahari yenye mawimbi. Wateja walitoka mbali na karibu kwa ajili ya mandhari hii tu.

“Hapa ndipo karibu zaidi na mbinguni,” kijana mmoja alimnong’oneza mpenzi wake walipokuwa wakitembea kwenye njia iliyoangazwa na mwezi kuelekea mkahawa uliokuwa umening’inia kwenye eneo la kutazamia juu ya kilele kirefu zaidi.

Kulikuwa na baridi kidogo hewani, baridi ambayo kikombe cha chai kingeweza kuiondoa haraka.

Mhudumu mpole alikuja kuchukua oda ya wanandoa hao. Tabasamu lake liliwafanya wajisikie wachangamfu na kukaribishwa.

“Ana, umeacha sahani hii nje. Nilikuambia ni lazima isafishwe,” ilisema sauti iliyokata zaidi ya ile baridi.

Yule mhudumu mkarimu alitetemeka.

“Nitarudi na chai yenu,” alitabasamu.

Wakati huo huo mwezi ulichomoza juu ya kilele cha mbali zaidi.

Mpenzi wa yule kijana alishtuka kwa mshangao.

“Huu ndio mwezi mkubwa zaidi niliowahi kuuona.”

Mpenzi wake wa kiume alimshika mkono mpenziwe kwa uchangamfu walipokuwa wakifurahia mandhari.

“Nilikuambia, ni lazima usikilize. Hakuna kisingizio, Ana. Na ukimaliza, fagia baraza. Kutakuwa na wageni wengine.”

Ile sauti ilikata katikati ya ule ubaridi kama kisu.

Yule mhudumu mkarimu alitokea na vikombe viwili vya chai ya moto.

“Karibuni,” alisema kwa tabasamu la upole, chozi likiwa limekwama kwenye kona ya jicho lake.

“Mwezi mrembo usiku wa leo,” aliwaambia wale wanandoa.

“Mwezi mrembo kuliko yote niliyowahi kuiona,” alijibu yule mpenzi wa kike.

“Ana!” ilipiga kelele sauti kutoka nyuma.

Mhudumu alitetemeka tena.

“Laiti usingekuwa mwezi mpevu,” alinong’ona yule mhudumu akijisemea. “Huibua mbwa mwitu ndani ya wengine.”

“Ana!” mama yake alipaza sauti. “Sivyo tena!”

A story by Pemba Umoja