Wewe Ni Mlima Wangu
Unapendwa ukiwa mbali, umebebwa katika ndoto
Ninakupenda
kama vile ninavyopenda milima
kwenye upeo wa mbali
Siwezi kuishi juu yake
Lakini ninaweza kuipenda nikiwa mbali
Naweza kuigusa kwa muda mfupi tu
lakini siwezi kupumzika nayo milele
Huo ndio umilele wetu
Kuheshimiwa kutoka mbali
Kukumbuka kukumbatiana
Kuishi katika kumbukumbu tulizowahi kushiriki
Siwezi kukuchukua nyumbani. Wala wewe mimi. Kama vile siwezi kuchukua mlima nyumbani
Labda wewe ni mkubwa sana kwa moyo wangu. Mkubwa mno kwa utaratibu wa maisha yangu
Wewe ni mlima unaoonekana tu juu ya mawingu. Katika ndoto na ukungu
Mwenye nguvu kiasi hiki kwenye moyo wangu
Ningeweza kuganda.
Viungo vingeweza kuanguka.
Ningeweza kutumbukia kwenye vilindi vilivyoganda
Kama ningekufa kwenye miteremko yako, nikiota moyo wako wenye joto, tabasamu lako la upole, kicheko chako cha utukutu
Labda furaha yangu, nyakati zetu, zingeganda katika umilele
Ninaomboleza maisha ya mlimani yaliyotarajiwa
Ambayao sitawahi kujua
Wewe ni mlima wangu
Mkubwa sana kwa maisha yangu
Lakini sitaacha kamwe kutazama upeo wa macho
Kwenye vilele
Vilivyo mbali sana na uwezo wangu
Mlima ule
ni wewe
A poem by Pemba Umoja