Mnong'ono
Kama mnong'ono angani
Nauona mwezi
siku za jua
Kama mnong'ono angani
Uliojificha nyuma ya bahari ya samawati
Ushawahi kuota unatembea peku juu ya vumbi la mwezi?
Ukitafuta oasisi inayoakisi nyota?
Sote tunahisi joto la nyota ileile
Na kutembea kwenye mawimbi ya mwezi
Kama wazazi angani
Hawakemei kamwe
Hawatuachi kamwe.
Daima waking'aa
Daima wakimetameta
Hata nyuma ya mawingu
Hata pale
tusipoweza tena
kuwaona.
A poem by Pemba Umoja