Kwenye Ncha za Vidole
Aliyaacha maji kama mtu amwachavyo mpenziwe.
Alitoka majini kwenye ncha za vidole
kana kwamba hakutaka kuondoka.
Kwa hakika,
alikuwa amechoka.
Alikuwa ameoga,
amelowa,
amecheza na mawimbi
kwa muda mrefu mno.
Ngozi yake ilikunjamana
na kusinyaa
kwa kupigwa na mawimbi.
Pumziko lilingoja
ufukweni,
ndani ya mchanga laini.
Lakini, ole!
mawimbi bado yalikuwa yakimwita.
Ingawa alitoka majini kwenye ncha za vidole,
alisita,
akayasikiliza mawimbi,
akageuka,
na kwa tabasamu,
akarejea baharini.
A poem by Pemba Umoja