Mawazo Yake
Moyo usiotaka kufunguliwa
Yeye ni msanii
Yeye ni mpenzi
Yeye ni ulimwengu wangu
lakini anaishi katika mwingine
Simjui kwa kweli
Labda sitamjua kamwe
Je, yeye ni ndoto tu,
fikira tu?
Je, nilimwumba mimi,
sehemu halisi,
sehemu ya milele?
Haijalishi
Anauvuta moyo wangu
anauchokoza
anaung'oa
kwenye komeo
lakini haufunguki.
A poem by Pemba Umoja