Dunia Bilioni 8
Nani kasema kuna sayari 8 tu angani?
Wakitembea njiani na vichochoroni
Wakitembea kutoka vitandani, na kuvirejea
Dunia za ndani
Mawazo na mahangaiko
Matumaini na ndoto
Wanafikiri kwa macho yao
Wakienda kushoto, kulia, kushoto, kulia
Ukitazama kwa muda mrefu, utaona
Nani kasema kuna sayari 8 tu angani?
Wakati kuna bilioni 8 duniani
Na bado hatujazungumzia marafiki zetu wenye manyoya
na wale wasumbufu wenye miguu 100
Usisahau ulimwengu wa juu
ulimwengu unaotuzunguka
ulimwengu wa ndani.
A poem by Pemba Umoja